Saturday, 16 September 2017

Partnership Deed Template


The Partnership Deed is a legal document addresses the rights and obligations of the parties to the partnership. This is like a constitution which shows the direction on how the partners under the partnership should regulate themselves.


On other way we can say this document is the contract whereby the partners are bound to follow. Because the partnership does not have a legal personality the mistake of single partner may affect the rest of partners in one way or another, therefore it is better the deed to be drafted well to cover all important details touch their partnership. Herein under is template of the Partnership Deed



PARTNERSHIP DEED

 THIS PARTNERSHIP DEED is made at Dar es salaam on this.........day of.........2017


BETWEEN


Comfort M. Ngowi of Po Box……………………………………(hereinafter referred as a PARTNER) on the one part


AND


Faith M. Ngowi of Po Box ……………………………………..(hereinafter referred as a PARTNER) on the other part


WHEREAS Partners are hereby agreed to be bound by terms provided under this Partnership Deed as follow: 


1. INTERPRETATION


In this paragraph some terms relating to the deed may be defined. These terms are those which might arouse ambiguities at the future; therefore it is necessary for them to be defined on how they are going to be used. This part is not necessary if such kinds of terms are not there.  


2. PARTIES


Here you have to provide names of parties under the Partnership Deed. You may also add a sentence explaining on how a person who wishes to join the partnership can do. Remember the partnership can comprise more than two members.


In the deed you can put the following words 'That the parties to this partnership are Comfort M. Ngowi and Faith M. Ngowi. Therefore the partner may agree to join any person to the Partnership after meet certain provided qualifications.


If there is a Partner who is a minor  then his parent or guardian who reaches the age of majority can be a partner instead of him temporarily until that minor turns eighteen (18) years.  



3. NAME OF BUSINESS


Under this paragraph you have to provide the name of the business. The business name is a trade name partnership going to use in conducting business. Example, under this clause you may put like this 'That the Partnership business name is so and so' 


4. OBJECT OF THE PARTNERSHIP 


What the partnership is made for? Here you have to provide the target of forming a partnership. You can say 'That the object of partnership agreement is doing a Poultry Business'


5. CAPITAL


This is money or properties brought in the partnership by partners. In capital clause you may show the percent or amount or share of each partner contributed to it. Example you may wish to say 'That in this partnership Comfort M. Ngowi has contributed 20 Million Tanzania Shillings while Faith M. Ngowi contributes 60 Million Tanzania Shillings.


However, not all kind of partnership partners going to contribute in terms of money. For instance, in Poultry farming business i have referred above one partners may contribute in terms of properties or one of them contribute the money and other properties, or both of them contribute both, money and properties.


Likewise in this clause you may provide details on what if at the future a capital would be required? Also which amount each partner is going to contribute. 


6. BUSINESS PLACE 


This clause should explain the place where a partnership business is going to be conducted. You may put in this way 'That the partnership business shall be carried out at Msoga Plot No. so and so Bagamoyo, Pwani.'


7. MANAGEMENT AND DECISION MAKING


How the management of the partnership will be conducted also how decision should be done. For example, date, time and place where partnership meeting should be conducted whether at the partnership premises or somewhere else, Coram when decision is made does it require consent of all partners?, or things relating to how to deal with partnership Bank account. 


8. PARTINERS DUTIES AND RESPONSIBILITIES


In this paragraph the duties and responsibilities of the partners in the partnership should be covered. Examples:  the partners should be doing the business in good faith, the partners is duty bound not to disclose confidential information to any parson relating to the partnership, or every partner has responsibilities to attend a business of the partnership.



9. PROFIT AND LOSSES 


The profit and losses of the partnership will be distributed to the partners equal to the proportion of their shares. This is done at the end of financial year of the partnership business.


10. ACCOUNTING RECORDS


Records relating to accounts of the partnership shall be kept at the business premises. The nature of those records shall be in the manner similar to those engaged on the same kind of the business.


11. LOANS TO THE PARTNERSHIP


The loans to the partnership paragraph should provide all details concerning the loans which may be taken for the partnership business. A loan may be taken to the bank after partners agreed or any partner may advance any sum to the partnership that will be out of his share to the partnership and he should be paid in the agreed rate. 


12. DETERMINATION OF PARTNERSHIP


At this paragraph you are going to give an explanation on how the partnership will come to an end. Example; if a partner dies, when a partner suffered an illness or injury which prevent him to participate into the partnership business to the certain period of time, serious breach the terms of this deed, failure to account for the money he has received to the business transactions relating to the partnership, when partner declared bankrupt, if the partner convicted with serious offence, or if fail to pay the money he owed by the partnership within certain period of time.


13. RESTRICTIONS


This section is going to impose restrictions to the partners regarding some actions. For instance, restrictions may be not to employ or dismiss an employee of the partnership without partner’s full consent, not to lend the partnerships money to any person, not to become a guarantor of any person, not to divulge any confidential information of partnership to the person who is not required to have it, not to deal with Bank account of partnership in other way than the accepted one under the deed, or not to be involved to any other business or occupation than the partnership business. 
  

14. DISPUTE RESOLUTION


This is a forum to take a matter when the dispute arises concerning the partnership. The parties may agree to take a matter directly to the Arbitrator instead of Court.


15. APPLICABLE LAW


If the deed involves partners from several jurisdictions then they may agree also which law should be used. 
  

IN WITNESSETH WHEREOF the parties hereto have executed these presents on the day and date first above written.


SIGNED and DELIVERED at.... by the said}
.......who is personally known to me in}                          

my presence this.........day of........}               PARTNER                              

Name: ..................................

Signature:..............................

Postal Address: ........................

Qualification: .........................



SIGNED and DELIVERED at.....by the said}

.......who is personally known to me in}                         
 my presence this.........day of.......}               PARTNER                           

Name: ..................................

Signature: .............................

Postal Address: ........................

Qualification: .........................

Sunday, 10 September 2017

Jinsi gani uandike mkataba?



Mkataba ni makubaliano baina ya watu au pande kadhaa yenye nguvu kisheria. Mkataba unaweza kuwa  wa maandishi, mdomo au vitendo. 

Mkataba wa maandishi ni aina ya makubaliano yanayoweza kufikiwa na kuwekwa katika mfumo wa kimaandishi. Katika aina hii ya mkataba ni vyema kabisa mambo ya msingi katika makubaliano yakajumuishwa ndani. Kanuni za kiuandishi ni sharti zizingatiwe ili kuondoa utata unaoweza kujitokeza mbeleni kwenye tafsiri.


Mkataba wa mdomo unaweza kufanywa kwa maneno ya mdomo. Kwa mfano unapokwenda dukani kwa Mangi mtaani kununua bidhaa fulani fulani za rejareja huwa hamuandikishiani bali mnakubaliana kwa njia ya mdomo.

Lakini pia tunapopanda daladala ili kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine hatuandikishani mkataba na makondakta bali huwa makubaliano yanafanyika kwa njia ya mdomo kwamba anakufikisha sehemu fulani kituoni unashuka halafu unamlipa nauli. Hii ni baadhi  ya mifano kadhaa ninayoweza kukupa kuhusiana na aina hii ya mkataba.
  

Mkataba wa vitendo ni mkataba amabao unaoweza kufanywa kwa njia ya matendo. Kwa mfano msambazaji wa mchele wa jumla kama kwa kawaida huwa analeta gunia kadhaa za mchele  na anamwachia muuzaji hafafu muuzaji akimaliza kuuza anamlipa yule msambazaji japokuwa hawakuandikishiana popote makubaliano yale yatakuwa na nguvu kisheria kwani mkataba ule tutauita  mkataba au makubaliano ya vitendo (implied contract).


Ni upi mkataba wenye nguvu kisheria? 


Maelezo ya hapo juu yanaweza yakawa ni makubaliano tu na sio mkataba. Ijulikane ya kwamba mikataba yote ni makubaliano ila sio makubaliano yote ni mikataba isipokuwa yamekidhi vigezo vya kimkataba. Vigezo hivyo  vimewekwa na sharia ya mikataba ya Tanzania kwa jina la The Law of Contract Act, [R.E 2002]. Kwenye kifungu cha 10 cha sharia hiyo kinataja baadhi ya vigezo ambayo ni lazima yawepo kwenye makubaliano fulani ili yaweze kuwa mkataba.

Vigezo hivyo ni kama vile lazima kuwe na makubaliano huru baina ya pande zinazohusika katika mkataba. Na makubaliano hayo hayapaswi kufikiwa kwa kushawishiwa na rushwa, kulazimishwa au nguvu.

Lakini pia wahusika wa mkataba ni sharti wawe na uwezo kisheria wa kuingia mkataba. Uwezo wa kisheria unaohitajika ili mtu aweze kuingia mikataba ni kama vile kutimiza umri wa miaka kumi na minane (18) au zaidi na asiwe na tatizo la akili wakati wanaingia makubaliano hayo kwa kiasi ambacho kitaathiri kuingiwa kwa mkataba.

Mkataba pia usiwe na lengo linalokwenda kinyume cha sharia au sera za nchi. Huwezi kufanya mkataba wa kuuziana bangi au dawa za kulevya au kuua mtu au kuuza mwili kingono ukadhani utakuwa na nguvu kisheria, haitowezekana kamwe kwani lengo lake linakwenda kinyume kabisa na sheria au sera za nchi.

Kigezo kingine ni lazima katika mkataba kuwe na mabadilishano ya kitu kwa kitu yanayoruhusiwa na sharia (a lawful consideration). Kwa mfano unapokwenda kununua nyumba kwa kiasi cha shilingi milioni kumi, tunasema hiyo milioni kumi ni consideration ya thamani ya nyumba. Hivyo ni baadhi ya vigezo vichache vinavyotakiwa ili makubaliano yawe mkataba.

Ndugu msomaji wangu pengine unaweza kujiuliza ni nini basi maana ya makubaliano? Na ni kwanini sio makubaliano yote yanaweza kuwa na nguvu kisheria au kuitwa mkataba? Nitalijibu swali hili kwa mifano.

Tuchukulie unae mtoto anasoma kidato cha nne na ukamuahidi simu aina ya SAMSUNG NOTE 5 endapo ataweza kufaulu mitihani yake ya kidato cha nne, ni wazi kabisa haya ni makubaliano tu kati ya mzazi na mwanawe na mtoto hatoweza kwenda kufungua shauri mahakamani kumshtaki mzazi wake kwa sababu hayajaweza kukidhi baadhi ya vigezo vinavyotakiwa na sheria ili yaweze kuwa mkataba. 

Mfano wa pili ni mume anaweza akamuahidi mkewe kumnunulia gari katika sherehe ya kukumbuka siku yake ya kuzaliwa, haya pia ni makubaliano yasiyoweza kufikia uwezo wa kuitwa mkataba kwani mume akishindwa kutimiza alichokiahidi mkewe hawezi kumshtaki mumewe kwa kuvunja mkataba kwani huo haujatimiza vigezo vya kuitwa mkataba.


Jinsi ya kuandaa mkataba wa biashara


Haya ni baadhi ya mambo yanayopaswa yawepo wakati unaandika mkataba wa biashara. Nomba ijulikane kwamba hakuna namna maalumu ya kuandika (draft) mkataba isipokuwa yapo mambo muhimu yanayoyakiwa yawepo katika mkataba:


1. Kichwa cha mkataba.


Huwa kinatangulia mwanzo wa mkataba kabla ya mambo yote. Kichwa cha mkataba kinaweza kuwekwa juu kabisa ya mkataba katikati kama ukipenda. Kichwa cha mkataba kinatakiwa kueleza mkataba huo unahusiana na nini kwa ufupi sana. Kinaposomwa kichwa cha mkataba picha ya mkataba mzima inatakiwa ionekane bila hata ya kuusoma ndani. Mfano inaweza ikawa hivi MKATABA WA MAUZIANO YA NYUMBA


2. Taja majina ya wahusika wa mkataba 


Baada ya kichwa cha mkataba unaweza ukaandika majina ya pande zinazohusika katika mkataba. Kumbuka sio kila mtu anatakiwa kuingia kwenye mkataba kama nilivyokwisha kudokeza. Kwa mfano, muunganiko wa kichwa cha mkataba na majina ya pande husika zinaweza kuwa katika muonekano ufuatao:


MKATABA WA MAUZIANO YA SHAMBA

kati ya

COMFORT M. NGOWI (wa S.L.P 54 Marangu, ambapo kwenye mkataba huu atajulikana kama ‘Muuzaji’)

na

FAITH M. NGOWI (wa S.L.P 432 Mabibo, ambapo katika mkataba huu atajulikana kama ‘Mnunuaji’)


3. Tarehe na mahali mliposainishana mkataba


Hii pia ni shehemu muhimu sana. Ni vyema tarehe ya siku mnayosainishiana mkataba ikawepo bila kusahau mahali. Inaweza ikawa ni mji au wilaya. Mfano: Mkataba huu umefungwa hapa DAR ES SALAAM leo Tarehe 21.08.2017.


4. Siku ya mkataba utakapoanza na kufikia ukomo rasmi


Kama mkataba unategemewa kuanza siku tofauti na ile ambayo wahusika wamesainishiana basi ni sharti kuwepo kifungu kinachoonyesha hivyo. Hii inatokea pale wahusika wa mkataba hawataweza kuonana siku za usoni hivyo mnaweza kusainishana mkataba tarehe fulani halafu mnaweka na kifungu kinachoonyesha siku utakapoanza rasmi. 

Kwa kuongezea tu kama mkataba una siku ya kufikia ukomo ni vyema tarehe ikaandikwa japokuwa hii sio muhimu sana kwani zipo njia nyingine zinazoweza kuufikisha mkataba kwenye ukomo.


5. Kiwango cha fedha kinachotumika 


Kiwango cha fedha kinachotumika katika biashara ni lazima kitajwe. Kwa mfano: Unaweza kuandika hivi ‘Kwamba muuzaji kamuuzia mnunuaji nyumba iliyoko Mabibo yenye namba Mabibo- Mwananchi plot b/480 Ubungo kwa kiasi cha Shilingi za KItanzania Milioni 800.


6. Kitu kinachohusika katika biashara


Ni lazima mkataba utaje ni kitu gani kinachohusika katika biashara mnayoiingia mkataba. Ni vyema ukaweka taarifa zote ambazo unadhani ni muhimu zinazohusiana na kitu hicho.

Rejea kwenye mfano nilioutoa hapo juu ‘Nyumba’ ndio kitu kinachohusika katika biashara. Na kama ambavyo tulivyoweza kuona taarifa kuhusiana na nyumba hiyo zimetolewa kama vile namba ya kiwanja pamoja na sehemu kilipo. Hii itasaidia kuondoa utata pindi litakapotokea tatizo baadae.


7. Namna malipo yatakavyofanyika


Je unataka njia gani itumike katika kufanya malipo? Je ni kwa njia ya Benki au Mkono au M-Pesa au Tigopesa? Je unataka malipo yafanyikeje, yote kwa pamoja au kidogo kidogo? Je unataka ulipwe kwa kutumia pesa ya kitanzania au kigeni? Yote haya unaweza ukayaweka kwenye mkataba kama sehemu ya makubaliano yenu.


8. Sehemu ambayo mngependa mgogoro ushughulikiwe endapo utatokea


Hapa mnaandika ni wapi mngependa mgogoro ushughulikiwe pindi utakapotokea. Je mtapenda kupeleka mgogoro wenu mahakamani au kwenye mabaraza ya usuluhishi? Kama mmoja wenu ni raia wa kigeni je mngependa iwe nchi gani yenye mamlaka ya kushughulikia mgogoro wenu? Kumbuka kama mmekubaliana katika mkataba mgogoro utakapotokea upelekwe sehemu fulani hamna atakayeweza kufanya vinginevyo nje ya makubaliano yanu. 


9. Sheria ambayo mngependa itumike kusimamia mkataba wenu


Maelezo ya hapa yanakaribia kufanana na hayo hapo juu kwenye kipengele namba nane (8). Ni uamuzi wenu kuchagua mnataka sheria ipi itumike kusimamia mkataba wenu. Hii itakuwa ina nafasi sana kama mnaingia mkataba unaohusisha raia wa nchi zaidi ya moja.

10.   Mambo yatakayopelekea mkataba kuvunjika

Mnaweza mkaweka kifungu ambacho kinabeba mambo ambayo kama yakifanyika yatapelekea mkataba wenu kuvunjika. Ni vyema kila upande kwenye makataba ukaguswa kwa namna yake na mambo hayo. Kwa mfano, mnaweza kukubaliana ya kwamba mnunuzi kama akichelewa kufanya malipo kwa muuzaji kwa kipindi cha siku thelathini (30) basi atakuwa amevunja masharti mkataba automatic. 


11. Taarifa


Mnaweza pia mkaweka kifungu ndani ya mkataba ambacho kinatoa anuani ya kutumia taarifa na endapo kama ikitokea kuna taarifa yoyote ambayo inatakiwa kumfikia yeyote anayehusika na mkataba. Mnaweza mkaweka anuani ya sanduku la barua au barua pepe au namba ya simu kama mtakavyokubaliana kwa kila upande. 


12. Mkataba unatakiwa usainiwe na wahusika katika mkataba


Kusaini mkataba ni ishara ya kwamba wahusika wote katika mkataba wamekubali kufungwa na yaliyomo ndani ya mkataba. Kabla hujasaini mkataba wowote sana sana ile inayoandaliwa na upande mmoja ‘standard form contract’ mfano wa ile tunayoiombea mikopo Benki uisome kwanza kwani kusaini mkataba kuna maana kubwa sana kuwa umekubali kubanwa na masharti yaliyomo ndani kama nilivyokwisha kuelezea, huwezi kusema baadae jamani sikusoma! utabanwa hata kama hukuusoma.


13. Mashahidi nao wanatakiwa kusaini


Hawa ni vizuri wasipungue wawili yaani mmoja kutoka kila upande. Hawa kazi yao ni kuthibitisha ya kwamba mkataba huu umesainiwa na wahusika mbele yao. Mashahidi wanatakiwa wawe ni watu wenye vigezo vya kuwa mashahidi yaani wasiwe watoto au watu wenye upungufu wa akili wakati wa kusaini mkataba.


Angalizo: Hivyo nilivyoviaja hapo juu ni mfano wa mambo yale muhimu yanayotakiwa katika mkataba, hivyo basi pande husika katika mkataba mnaweza kukubaliana mnavyotaka isipokuwa vipengele vyenu visiende kinyume na sheria za nchi. Pia ijulikane ya kwamba mikataba inatofautiana. Ni wazi mkataba wa kuuziana gari hauwezi kufanana na ule ya kuuza au kukodisha nyumba. Kwa maana hiyo nilichokifanya hapa ndugu msomaji wangu ni kukupa mwanga namna mkataba unatakiwa kuandikwa vingine utajiongeza.